Posts

Showing posts from March, 2020
Image
MIRUNDIKO YA TAKA NAROK YAZUA HOFU KWA WAKAAJI. Imewalazimu wakaaji wa jijini Narok kuichukulia hali hii ya kuzungukwa na taka kawaida, kwani wametoa malalamishi yao kwa baraza la kaunti hii inayohusika na ukusanyaji wa taka bali ikawa bidii zao zimeambulia patupu. Hakuna wa kushughulika. Ni jambo la kutatanisha kwamba hata ingawa jiji hili la Narok ni lenye kazi sana,kiwango au urari wa uchafu wake umezidi ule wa maeneo ya mashinani katika kaunti hii. Kusongamana kwa watu ndio, kunachangia kuwepo kwa taka nyingi lakini pia kwa kuwajibika taka hizo zaweza kushughulikiwa kwa ufanisi ili kuzingatia usafi ambao ni muhimu zaidi ya mambo yote. Hali inayozua hofu zaidi na kuhatarisha afya ya wakaaji wa jiji na nje ya Narok ni kwamba hakuna hata angalau mapipa ambapo wanaweza tia taka zao. Hii inasababisha kusambaa kwa taka kila mahali,mitaro na hata barabara huwa mapipa yao. La kuhuzunisha pia ni kwamba hakuna atakayezoa taka hizo hapo, ni kazi ya maji ya mvua kubeba taka taka hizo h...
Image
MAHAFALI YA NANE;CHUO CHA UALIMU NAROK. Wanafunzi pamoja na waliohudhuria sherehe hii ya mahafali wakisubiri ianze katika Chuo cha Ualimu cha Narok Wanafunzi 614 wamehitimu leo hii kutoka Chuo cha Ualimu ndani ya kaunti ya Narok ikiashiria kukamilisha masomo rasmi na kujiandaa kwa ajili ya kulitumikia taifa hili. Kwa miaka mwili au mitatu kulingana na kitengo cha kila mmoja,wanafunzi hawa walipata kuingia mwituni na leo hii ni wazi kwamba baadhi yao wamepata kurejea na kuni ambazo kwa hakika zitawafaidi pakubwa katika siku zao za usoni. Wanafunzi hao wakiwa katika kanzu za mahafali walionyesha furaha na kuridhika kwa siku hii walioisubiria bila ya kujuta tangu mwaka jana walipomaliza kuudhuria masomo yao. Wanatumaini kupata kazi kwa sababu wameshakabidhiwa vyeti vyao vya kuhitimu tofauti na vyuo vingine ambapo wanafunzi huchukua vyeti vyao baadaye mbali na siku yao ya kuhitimu. Cynthia Chemtai mmoja wa waliohitimu anasema, "sina shaka nitapata kazi maanake sifa zote na uj...